• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji la Dodoma laendelea na kampeni ya miti

Imewekwa tarehe: July 13th, 2019

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeanzisha kampeni ya upandaji miti katika jitihada yake za kulifanya jiji hilo kuwa la kijani na mahali salama pa kuishi watu wote.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi alipokuwa akiwasilisha utangulizi wa Mpango Kabambe wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma mbele ya kamati ya uwekezaji ya Bunge la Jumuiya ya Madola kanda ya Afrika waliotembelea jiji hilo kuangalia fursa za uwekezaji katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma jana.

Kunambi alisema kuwa katika kulifanya Jiji la Dodoma linakuwa mahali salama zaidi pa kuishi, Halmashauri yake imeanzisha kampeni kubwa ya upandaji miti katika maeneo mbalimbali. Alisema kuwa katika kutekeleza kampeni hiyo vikao vya maamuzi vimepitisha kuwa kila kaya itakuwa na wajibu wa kupanda angalau miti mitano kuzunguka eneo la kaya hiyo. “Tunataka ndani ya miaka minne ijayo Jiji la Dodoma liwe la kijani” alisema Kunambi. Aidha, aliongeza kuwa jiji hilo linajipanga kukabiliana na changamoto ya menejimenti ya taka ngumu. Alisema kuwa dhamira ya jiji hilo ni kufikia uwezo wa kutenganisha taka ngumu na taka nyingine na kufanya mchakato wa kuzichakata kuwa rahisi.

 Akiongelea eneo la uwekezaji, Mkurugenzi huyo aliwakaribisha wabunge hao kuwekeza katika kilimo cha zabibu na uchakataji wake. “Katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma mnakaribishwa kuwekeza katika kilimo cha zabibu na mazao mengine” alisema Kunambi. Vilevile, alisema kuwa Halmashauri hiyo imeandaa na kutenga maeneo mengine kwa ajili ya uwekezaji katika viwanda kwa ajili ya matumizi mbalimbali.

Akiongelea miundombinu, alisema kuwa barabara za ndani ya jiji zinaendelea kujengwa kwa ajili ya kuunganisha na kuboresha miundombinu hiyo kwa wananchi. Alisema kuwa nia ya jiji hilo ni kuunganisha mtandao wa barabara, reli na anga. “Uwanja wa Ndege wa Msalato unatarajiwa kujengwa ndani ya muda mfupi. Usanifu wake umekamilika na kazi ilifanywa na kampuni kutoka nchini Tunisia. Kwa mujibu wa Mpango kabambe wa Halmashauri ya Jiji, tutaunganisha uwanja wa Ndege uliopo karibu Km 30 kutoka mjini kati na reli ya umeme ya kisasa (SGR) itakayotokea Dar es Salaam kuja Dodoma. Mradi unaoendelea na unatarajiwa kukamilika mwaka 2021. Baada ya kukamilika mtu atakuwa na uwezo wa kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma kwa kutumia masaa matatu pekee” alisema Kunambi.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.