• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji la Dodoma lampongeza Rais kwa kuboresha miundombinu ya elimu ya awali na msingi

Imewekwa tarehe: May 27th, 2023

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imetoa shukrani kwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha miundombinu ya elimu ya awali na msingi kwa kuwahakikishia wanafunzi mazingira bora ya kujifunzia.

Shukrani hizo zilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Elimu ya awali na msingi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prisca Myalla alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu chini ya mradi wa kuboresha upatikanaji wa fursa sawa katika ujifunzaji bora wa elimu ya awali na msingi Tanzania bara (BOOST) kwa shule ya msingi Chang’ombe na Swaswa katika Jiji la Dodoma.

“Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha miundombinu ya elimu ya awali na msingi kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Miundombinu hii imekuwa chachu ya maendeleo ya elimu na taaluma. Leo nimetembelea kukagua maendeleo ya ujenzi katika shule ya msingi Chang’ombe. Ujenzi katika shule hiyo upo katika hatua nzuri. Wapo hatua ya kupaua na tayari wameshapiga bati kwa baadhi ya maeneo ya madarasa. Na huko nimewasisitiza kuongeza kasi ili kukamilisha ujenzi kwa wakati.

Hapa Kata ya Ipagala inajengwa shule ya msingi Swaswa ambayo ni mpya kabisa. Kama tunavyoona ujenzi unaendelea ukiwa hatua ya lenta na mafundi wapo eneo la mradi. Nimewasisitiza kuongeza kasi ya ujenzi ili ifikapo tarehe 10 Juni, 2023 kazi iwe imekamilika” alisema Myalla.

Kwa upande wa Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Ipalaba B, Praxeda Fundisha alisema kuwa shule yake ilipokea shilingi 318,800,000 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa tisa, jengo la utawala na matundu 16 ya vyoo. “Kama mnavyojionea leo ni wikendi lakini mafundi wanaendelea na kazi wakifunga lenta na wengine wanafunga mbao za kenchi. Ujenzi wa shule hii utafanya kazi ya ufundishaji kwa walimu kuwa rahisi kwa sababu watoto watakuwa wamepungua darasani. Mfano shule ya Ipagala B, mkondo mmoja unafika wanafunzi 120 kwa darasa moja. Hivyo, kupungua kutakuwa kumewarahisishia sana walimu na wanafunzi ufaulu utapanda” alisema Fundisha.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Swaswa, Charles Nyuma alisema kuwa mtaa wake una wananchi wengi katika Kata ya Ipagala kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi iliyopita. “Tuna takribani wananchi 10,941. Mtaa wetu ulikuwa hauna shule ya msingi. Mtaa kilio chetu ilikuwa ni kupata shule ya msingi. Watoto wetu wanatembea umbali mrefu kwenda shule wakivuka mapori na makorongo jambo ambalo ni hatari kwao. Kwa kweli serikali ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan hakika tunaishukuru sana jinsi ilivyotupatia shule hii” alisema Nyuma.

Nae Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa shule ya msingi Swaswa, Samwel Bosco alimtaja Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa ameikumbuka sana sekta ya elimu. “Elimu ndiyo kila kitu kwa Maisha ya sasa na vizazi vijavyo. Tunategemea shule hii mwezi Julai, 2023 ianze. Tupo saiti tunafanya kazi usiku na mchana na tutahakikisha pesa inatumika ipasavyo bila hata msumali kupotea bali kutumika pale unapotakiwa kutumika” alisema Bosco.

Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilipokea shilingi 1,654,000,000 kutoka mradi wa BOOST kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya shule za msingi ikiwa ni ujenzi wa shule nne mpya na ujenzi wa madarasa kadhaa.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.