• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

TENT yaahidi kushirikiana na BMH kupandikiza ngoma za sikio

Imewekwa tarehe: November 27th, 2020

Madaktari bingwa na Wataalam wa magonjwa ya Sikio, Pua na Koo nchini (TENT) wameahidi kushirikiana na Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) kuanzisha huduma za upandikizaji wa Kifaa Maalumu cha Usikivu (Cochlear Implant) ili kuwasogezea huduma hiyo wananchi wa Kanda ya Kati.

Awali akifungua mkutano wa mwaka wa kisayansi wa Jumuiya ya Madaktari bingwa na Wataalam wa magonjwa ya Sikio, Pua na Koo unaoendela katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Dkt. Januarius Hinju, kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ametoa rai kwa wataalamu hao kutumia mkutano huo ili pamoja na mambo mengine wajadili namna bora ya kushirikiana kutoa huduma ya kupandikiza kifaa maalumu cha Usikivu (Cochlear), ili kuwapunguzia wananchi wa kanda ya kati usumbufu wa kufuata huduma hiyo Dar es Salaam

“kwa vile tumebobea katika huduma za kupandikiza viungo, na tuna vifaa vya kisasa kwa matibabu ya kibingwa ya magonjwa ya masikio, pua na koo, tunawaalika wataalamu wazawa wa magonjwa ya Sikio, Pua na Koo waje tushirikiane kutoa huduma za kibingwa za kupandikiza kifaa maalum cha usikivu, alisema Dkt. Hinju.

Aidha, Dkt. Hinju amebainisha kuwa Hospitali ya Benjamin Mkapa inazidi kuboresha huduma zake kwani ndani ya kipindi cha miaka mitano imeweza kutoa huduma za kupandikiza Figo kwa kutumia watalaam wazawa na kwa sasa iko mbioni kutoa huduma za upasuaji moyo kwa kufungua kifua (open heart surgery) pamoja na kupandikiza uroto.

Kwa upande wake Rais wa Jumuiya ya Madaktari bingwa na Wataalam wa Magonjwa ya Sikio, Pua na Koo (TENT) Dkt. Edwin Liyombo ameishukuru Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa mapokezi makubwa waliyopata na kuahidi kutumia mkutano huo kulifanyia kazi ombi la kushirikiana kutoa huduma za kibingwa za kupandikiza kifaa maalum cha usikivu kwa wananchi wa Kanda ya Kati.

“Kabla ya Mkutano huu nilikuja kutembea hapa BMH, hii hospitali iko vizuri, inavifaa vya kisasa kabisa, hata vifaa tiba vinavyotumika kwenye kliniki za ENT ni vya viwango vya kisasa vinavyotumika katika hospitali za Ulaya, TENT nchini tupo tayari kushirikiana nanyi wakati wowote” Alisema Dkt. Edwin.

Picha na matukio:





Chanzo: Wizara_afyatz

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.